• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ELIMU YA MATUMIZI BORA YA FEDHA YATOLEWA KWA WANUFAIKA WA MKOPO WA ASILIMIA 10

Posted on: January 18th, 2023

Jumla ya vikundi 37 vinavyonufaika na mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri ya manispaa ya Ilemela inayojumuisha asilimia 4 kwa ajili ya wanawake,asilimia 4 kwa vijana na asilimia 2 kwa watu wenye ulemavu vimepatiwa mafunzo sambamba na zoezi la ujazaji wa mikataba ya mikopo ambayo inatarajiwa kutolewa katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023.



Akizungumza wakati wa zoezi la kujaza mikataba na utiaji saini wa mikataba ya ukopeshaji fedha  kwa  vikundi hivyo lililofanyika katika ukumbi  wa manispaa ya Ilemela Afisa maendeleo wa manispaa ya Ilemela Bi Amina Bululu amewataka wana vikundi hao kuhakikisha wanatumia fedha hizo kwa ajili ya miradi iliyokusudiwa sanjari na kuhakikisha wanarejesha fedha hizo katika muda uliopangwa kulingana na mkataba bila riba yeyote.


“ Ni utaratibu wetu wa kawaida kutoa mafunzo haya ya kukumbushana matumizi bora ya fedha mnazokopeshwa hasa tunapokutana kwa pamoja kama hivi ili zilete tija katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mnazofanya na kufanya zoezi la kukopesha liwe endelevu.”



Aidha Bi. Bululu amevipongeza vikundi vya wanawake kwa marejesho mazuri ya fedha hizo za mkopo huku akiviasa vikundi vya vijana na watu wenye ulemavu kuhakikisha navyo vinarejesha kwa wakati ili viweze kupata fedha nyingi zaidi na kukuza biashara sambamba na kuongeza kipato chao.



Kwa upande wake afisa maendeleo ya vijana manispaa ya Ilemela Bi Lucy Nicholaus Matemba amevitaka vikundi vinavyokopeshwa na manispaa kuhakikisha vinayaishi makubaliano yaliyo katika mkataba pamoja na kusisitiza kuwa wasiache kuwatumia maafisa maendeleo walio katika maeneo yao au wale wa makao makuu ya wilaya pindi zinapojitokeza changamoto zozote.


Monika Makaranga ni mwenyekiti wa kikundi cha Tupendane group 2020 kilichopo Msumbiji kata ya Kawekamo kinachojishughulisha na ufugaji wa kuku ,usindikaji wa vyakula ambavyo ni viungo na unga wa lishe,kwa niaba ya kikundi chake ameishukuru Manispaa ya Ilemela kwa kukubali kuwapatia mkopo awamu nyingine wa shilingi milioni 10 ambayo wanatarajia kuitumia kwa mradi mpya wa bajaji.



Nae Bi. Judith Kasuja Joseph ambae ni mlemavu wa miguu kutoka kata ya Kahama mtaa wa Isela ameipongeza manispaa hiyo kwa uwepo wa masharti mepesi upande wa walemavu katika kupata mkopo.



Halmashauri ilitenga jumla ya kiasi cha shilingi milioni 285,000,000 inayotarajiwa kutolewa kwa vikundi 37 ndani ya manispaa ya Ilemela kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023.





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.