• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

'HAKI YA BINTI'- MRADI MPYA KATIKA MANISPAA YA ILEMELA

Posted on: July 30th, 2020

Shirika lisilo la kiserikali la WADADA linaloshughulika na masuala ya mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia,ulinzi na utetezi wa haki za watoto na mabinti  limetambulisha mradi wake mpya unaotambulika kwa jina la “HAKI YA BINTI”kwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela.


Mradi huu unatarajia kufanya kazi ndani ya Manispaa ya Ilemela ukihusisha kata mbili Kitangiri na Pasiansi ambapo wadau na wataalam mbalimbali wa afya, elimu ,vyombo vya ulinzi na usalama watahusishwa.


Akiutambulisha mradi huo mpya, Mwenyekiti wa bodi, Ndugu Amri Linus alisema kuwa, anategemea kuwa jamii nufaika inapata mabadiliko makubwa kwa kuangalia namna wanavyoweza kujikinga na ukatili wa kijinsia pamoja na kuhakikisha kuwa jamii inapata uelewa wa nini maana ya haki ya binti.


Bi.Anitha Samson ambae ni mratibu mradi amesema mradi utahusisha mabinti kuanzia  umri  miaka 7 mpaka 25 ambapo lengo kuu la mradi ni kuwajengea uwezo mabinti katika kupambana na matukio ya ukatili na unyanyasaji ndani ya jamii.

“Tunatamani mabinti wote wawe na uwezo wa kutambua na kupaza sauti zao pindi wanapoona viashiria au wanapofanyiwa ukatili wa aina yoyote ile,lakini pia wawe msaada kwa wengine wasioweza kuzungumza kwa kuwaelewesha na kuwasemea.”amesema


Sambamba na hilo Bi.Anitha amesisitiza kuwa wamejipanga katika kuwawezesha mabinti kiuchumi ,kutoa elimu ya stadi za maisha na elimu ya ujasiliamali kulingana na mzingira waliopo,ili waweze kujisimamia na kuendesha maisha kwa kujiamini na kuepuka vishawishi.


Nae Mkuu wa Idara ya maendeleo ya jamii ndugu Sitta Singibala amelishukuru shirika la WADADA kwa ujio wa mradi huo ndani ya Ilemela.


“Natambua kuwa nyie ni wadau wetu kwa muda mrefu sasa na kazi zenu nyingi zinaendelea kuleta matokeo mazuri maeneo mlikopita kwani kumekuwa na ongezeko la uelewa kwa jamii juu ya mapambano dhidi ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia.Tunajivunia shule ya sekondari Mihama kwa uthubutu wao katika kuhamasisha jamii juu ya kutonyamazia matukio ya ukatili”


Aidha Mkurugenzi wa shirika la WADADA Bi.Ruth John ameitaka jamii ya Ilemela hashasa mabinti kujitambua na kuwa huru kuwaona punde wanapoona matukio ya ukatili.


“Mabinti zetu wa Ilemela tunawapenda sana ,tupo kwa ajili yenu msisite kutufikia kwa ushauri au msaada wa kisheria katika masuala mbalimbali ya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji.”alisema


Akihitimisha zoezi hilo la utambulisho wa mradi, mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ndugu Godfrey Mzanva ambae ni Afisa Tarafa wa Ilemela amesema

“Ni wajibu wetu kuwatambua, kuwafikia na kuwalinda mabinti wote.Kusiwe na “gap”kati ya walimu na watoto mashuleni.Walimu na wazazi watambue kuwa wanapaswa kuwa marafiki wa watoto na wawalee katika mazingira rafiki ya kumfanya mtoto kuwa huru kutoa changamoto zake. Jamii ya Ilemela tusinyamaze pindi tunapoona matukio ya ukatili wa kingono na ukatili wa aina yoyote ile ndani ya jamii yetu.Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vipo tayari kutoa ushirikiano na kutokomeza kabisa ukatili ”


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.