• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI, WITO WATOLEWA KUTOZALISHA HOJA MPYA ZA UKAGUZI

Posted on: June 17th, 2025

Mhe Said Mtanda, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ameipongeza Manispaa ya Ilemela kwa kuendelea kupata hati safi kwa mara ya tano mfululizo, huku akiitaka manispaa hii kuhakikisha haizalishi hoja mpya za ukaguzi kwa kuzijibu kwa wakati, ili ziweze kufungwa.

 

Ameyasema hayo mbele ya mkutano wa baraza la madiwani ulioketi tarehe 17 juni 2025 kwa ajili ya kupokea na kujadili hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024 pamoja na utekelezaji wake.

 

"Tuendelee kuhakikisha hatuzalishi hoja mpya za ukaguzi kwa kujibu kwa wakati, na zifungwe ili tusizalishe hoja mpya, pamoja na kutekeleza kikamilifu maoni ambayo yanatolewa na CAG sambamba na kushirikiana nae ili kuendelea kuzipatia majibu hoja hizo"

 

Aidha Mhe Mtanda amesisitiza juu ya ushiriki wa idara zote kikamilifu wakati wa kujibu hoja hizo zinapojitokeza, "hii ni halmashauri na sio kampuni ya mtu binafsi idara zote ni lazima zishirikishwe pale hoja zinapojitokeza", amesisitiza.

 

Akiwasilisha majibu ya ukaguzi huo, Ndugu Richson Ringo ambae ni mkaguzi mkuu wa nje wa mkoa wa Mwanza amesema kuwa katika mwaka 2023/2024 manispaa ya Ilemela ilipata hati safi (unqualified opinion).

 

Aidha ndugu Ringo amesema kuwa sababu iliyopelekea hoja au mapendekezo yaliyosalia kutokufungwa inatokana na kukosekana kwa mikakati thabiti na ya dhati kwa watekelezaji pia kutokushirikishwa ipasavyo kwa wakuu wa idara wanaohusika na hoja hizo, sambamba na majibu ya menejimenti yanakosa vielelezo na ushahidi wa kutosha ili kuwezesha kufungwa kwa hoja hizo.

 

Mariam Mshana, ni mweka hazina wa manispaa ya Ilemela akiwasilisha taarifa ya hoja zilizojitokeza kwa niaba ya mkurugenzi amesema kuwa, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 halmashauri ya manispaa ya Ilemela ilikutwa na hoja 42 ambapo hadi sasa hoja 30 zimefungwa na hivyo kubakiwa na hoja 12 ambazo zipo katika utekelezaji ikiwa ni sawa na asilimia 71  ya hoja ambazo zimefungwa .

 

Vilevile, Bi Mariam amesema kuwa kwa kipindi cha miaka mitano (5) mfululizo kuanzia mwaka 2019/2020, 2020/2021, 2021/2022, 2022/2023 na 2023/2024 halmashauri ya manispaa ya ilemela imeendelea kupata hati safi na kubainisha kuwa sababu iliyopelekea kupata hati hiyo ni ushirikiano baina ya wataalam, waheshimiwa madiwani, ofisi ya mkuu wa wilaya na ofisi ya mkuu wa mkoa katika kuhakikisha halmashauri inaendeshwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu. 

 

Nae mbunge wa jimbo la Ilemela, Mhe Dkt Angeline Mabula amepongeza kwa kazi nzuri inayoendelea kutekelezwa na watendaji wa ilemela chini ya mkurugenzi,  huku akihoji juu ya hoja nne ambazo zipo katika utekelezaji na hazijafungwa ambapo alitumia fursa hiyo kumuomba mkuu wa mkoa kutatua juu ya suala la hoja ya ardhi kuuzwa na jiji la mwanza ikiwa ipo kwenye ardhi ya manispaa ya ilemela pasipo kuishirikisha manispaa ya ilemela.

 

Kila baada ya mwaka wa fedha kuisha, halmashauri zinapaswa kuwasilisha taarifa zake za hesabu kwa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa ajili ya ukaguzi na baada ya kufanyiwa ukaguzi, halmashauri hupewa nafasi ya kujibu hoja zake na ukaguzi huu hufanyika kwa mujibu wa sheria ya fedha ya serikali za mitaa (Local Government Finance Act, 1982), iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019, 

 

 

 

 

 

 

Announcements

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • CHANJO YA KUKU KUWANUFAISHA WAFUGAJI

    July 09, 2025
  • PROF NAGU AMEWATAKA WATUMISHI KADA YA AFYA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    July 08, 2025
  • WALIMU WA AJIRA MPYA WAMETAKIWA KUWEKA MIPANGO SAHIHI YA KAZI

    July 04, 2025
  • ELIMU YA FEDHA KUWAONGEZEA UFANISI WANUFAIKA WA TASAF

    July 03, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.